Ikumbukwe kwamba, bajeti ya mwaka 2019/20 ilipitisha masuala mbalimbali na Kituo cha Sheria kama mdau kilifanya uchambuzi na kubaini masuala yenye maslahi ya haki za binadamu kama ifuatavyo;
Bajeti ya 2019 ilipunguza ushuru wa forodha kutoka asilimia 10 hadi asilimia 0 kwenye malighafi ya kutengeneza taulo za watoto (Baby Diaper) zinazotengenezwa nchini kwa mwaka mmoja.
Ni imani yetu kwamba, bajeti ya mwaka 2020/2021 itaendelea kulinda kipengele hiki kwa kujali ustawi wa afya ya mtoto. Pia, Serikali iimarishe mifumo ya ulinzi wa mtoto kwa kuzingatia changamoto zinazowakumba watoto nchini. Kwa mujibu wa Ripoti ya Haki za Binadamu ya 2019 iliyotolewa na LHRC imeanisha jumla ya visa 14,419, vya matukio ya ukatili dhidi ya watoto.
Bajeti ya 2019/20 ilipunguza ushuru wa forodha kutoka asilimia 25 hadi asilimia 0 kwa mwaka mmoja kwenye vifungashio vya mbegu vianavyotumiwa na wazalishaji wa mbegu hapa nchini. LHRC inatoa wito kwa Serikali kuendeleza punguzo hili la ushuru wa forodha ili kuendelea kuhamasisha uchumi wa wakulima katika mwaka wa fedha 2020/21.
Bajeti ya 2019/20 ilisamehe kodi kwenye mauzo ghafi yasiyozidi shilingi milioni nne (4,000,000/=) kwa wenye vitambulisho vya wajasiriamali na kupunguza kiwango cha chini cha kodi kutoka shilingi laki moja na nusu (150,000/=) kwa mwaka hadi shili laki moja (100,000/=) kwa mwaka. LHRC inatoa wito kwa bajeti ijayo iweke nafuu zaidi ili kusaidia kundi kubwa la wajasiriamali wadogo nchini.
Kupunguza ushuru wa forodha kutoka asilima 10 hadi asilimia 0 kwa mwaka mmoja kwenye machine za kielektroniki zinazotumika kukusanya mapato ya Serikali (Electronic Fiscal Device). Hatua hii ilikuwa hatua nzuri ya kupongezwa katika bajeti ya mwaka 2019/20, imesaidia kuhamisha mazingira mazuri ya ukusanyaji kodi.
Bajeti ya mwaka 2019/20 iliupunguza ushuru wa forodha kutoka asilimia 100 hadi asilimia 35 kwa mwaka mmoja kwenye sukari ya matumizi ya kawaida (consumption sugar) inayoagizwa kutoka nje ya nchi kwa vibali maalum kwa lengo la kuziba pengo la uzalishaji hapa nchini. LHRC inatoa wito kwa Serikali kuweka punguzo zaidi katika bajeti ya mwaka wa fedha 2020/21.
Kwa mwaka fedha 2020/21 LHRC inatoa wito kwa serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuzingatia masuala yafuatayo ili kulinda masuala ya haki za binadamu yanayotegemea hatua za kibajeti;
Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu kinaendelea kutoa rai kwa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kuzingatia hali ya ugonjwa wa corona katika kupitisha bajeti za wizara na taasisi mbalimbali ili ziendane na mapambano ya ugonjwa huu.
Soma hapa uchambuzi wa awali.
Imetoleawa Mei 22, 2020 na,
Kituo cha Sheria na Haki za Bindamu
Unleash your inner purpose to help the helpless, marginalized and oppressed. Your contribution will help our course in provision of legal aid and promotion of human rights.
Help us curb human rights violations such as the murderous attack against people with albinism and elders.
Your donation will help us empower the general public with civic education on cross cutting issues counting gender issues and democracy to realize the changes we aspire.
Help us safeguard human rights all together.
Huenda huna muda wa kutosha wala kipato cha kutosha kulinda utu na haki za wengine, ingawa unawiwa kufanya hivyo.
Ni jukumu letu sote kujitoa kwa kidogo tulichojaaliwa ili kupaka rangi ya furaha katika nyuso za wengine, wewe, yule na sisi tukikusanya nguvu tunaweza kutetea na kulinda haki za wanaoonewa kwa kushindwa kuzifikia huduma za haki.
Jitolee sasa kidogo ulichonacho kusaidia ulinzi na utetezi wa haki na utu wa binadamu.

LEAVE A REPLY
Your email address will not be published.