Tanzania imetangaza kupiga marufuku kutengeneza, kusambaza, kutumia au kutunza mifuko ya plastiki kuanzia tarehe 1 Juni mwaka 2019. Katazo hili linafuatia tangazo lililotolewa na Waziri Mkuu na Waziri wa Ofisi ya Makamu wa Rais anayeshughulikia Muungano na Mazingira. Katazo la mifuko ya plastiki ni utekelezaji wa kifungu cha 230 (2)(f) ya Sheria ya Usimamizi wa Mazingira ya mwaka 2004. Tangazo la katazo la mifuko ya plastiki limeanza utekelezaji kwa kutungwa kwa Kanuni husika za Usimamizi wa Mazingira za Kupiga Marufuku Mifuko ya Plastiki za mwaka 2019. Kanuni hizi zilitangazwa na Waziri wa Ofisi ya Makamu ya Rais Mambo ya Muungano na Mazingira, Mh. Januari Makamba ambazo zimeanza kutumika terehe 1 Juni 2019.
Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu kimefanya uchambuzi wa Kanuni hizo kama ilivyoambatanishwa hapa.
Tafadhali soma na usambaze kwa wengine.
Unleash your inner purpose to help the helpless, marginalized and oppressed. Your contribution will help our course in provision of legal aid and promotion of human rights.
Help us curb human rights violations such as the murderous attack against people with albinism and elders.
Your donation will help us empower the general public with civic education on cross cutting issues counting gender issues and democracy to realize the changes we aspire.
Help us safeguard human rights all together.
Huenda huna muda wa kutosha wala kipato cha kutosha kulinda utu na haki za wengine, ingawa unawiwa kufanya hivyo.
Ni jukumu letu sote kujitoa kwa kidogo tulichojaaliwa ili kupaka rangi ya furaha katika nyuso za wengine, wewe, yule na sisi tukikusanya nguvu tunaweza kutetea na kulinda haki za wanaoonewa kwa kushindwa kuzifikia huduma za haki.
Jitolee sasa kidogo ulichonacho kusaidia ulinzi na utetezi wa haki na utu wa binadamu.

LEAVE A REPLY
Your email address will not be published.