Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu kinalaani mauaji yaliyoripotiwa mkoani Mwanza katika wilaya ya Misungwi ambapo miili ya wanawake wanne wakazi wa vijiji vitatu tofauti ambavyo ni kijiji cha Isakamawe, Misasi na Mabuki imeokotwa Agosti 3, 2018. Kwa mujibu wa jeshi la polisi mkoa wa Mwanza mauaji hayo yanasadikika kuhusishwa na imani za kishirikina kwani miili ya wanawake hao imenyofolewa baadhi ya viungo ikiwemo viungo vya siri.
Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu kinalaani vikali ukiukwaji huo mkubwa wa haki ya kuishi. Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu kinatoa rai kwa wananchi kuheshimu na kulinda haki za binadamu hususani haki ya kuishi ambayo ni haki ya msingi zaidi kwa kila binadamu.
Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu kinawahimiza wananchi kutoa ushirikiano kwa jeshi la polisi ili kufanikisha zoezi la kuwatia hatiani wote walioshiriki ukatili huo. Pia, Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu kinatoa rai kwa Serikali kuimarisha mifumo ya ulinzi na usalama kwa wananchi ili kuepuka vitendo vya kikatili vinavyozidi kushamiri nchini.
Imetolewa Jumamosi Agosti 4, 2018 na;
Bi. Anna Henga (Wakili)
Mkurugenzi Mtendaji
Your email address will not be published.
Unleash your inner purpose to help the helpless, marginalized and oppressed. Your contribution will help our course in provision of legal aid and promotion of human rights.
Help us curb human rights violations such as the murderous attack against people with albinism and elders.
Your donation will help us empower the general public with civic education on cross cutting issues counting gender issues and democracy to realize the changes we aspire.
Help us safeguard human rights all together.
Huenda huna muda wa kutosha wala kipato cha kutosha kulinda utu na haki za wengine, ingawa unawiwa kufanya hivyo.
Ni jukumu letu sote kujitoa kwa kidogo tulichojaaliwa ili kupaka rangi ya furaha katika nyuso za wengine, wewe, yule na sisi tukikusanya nguvu tunaweza kutetea na kulinda haki za wanaoonewa kwa kushindwa kuzifikia huduma za haki.
Jitolee sasa kidogo ulichonacho kusaidia ulinzi na utetezi wa haki na utu wa binadamu.

1 COMMENTS FOUND
Mtani Says:
September 9th ,2018 9:42 PMHello i NEED HELP OF A LAWYER!