Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu kimepokea kwa masikitiko taarifa ya kushambuliwa na kuuawa kwa maafisa watatu wa Jeshi la Polisi katika wilaya ya Uvinza mkoani Kigoma. Katika taarifa hizo, mnamo Oktoba 16, 2018 Mkuu wa Kituo cha Polisi Nguruka , wilaya ya Uvinza mkoa wa Kigoma, Bwana Ramadhani Mdimi pamoja na askari wengine wawili waliuawa wakati wakitekeleza zoezi la kuwaondoa wananchi wanaosemakana kuvamia eno la ufugaji la Ranchi ya Taifa NARCO na kufanya shughuli za kilimo kinyume na sheria. Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu kinatoa pole kwa Mkuu wa Jeshi la Polisi na familia za askari waliouawa.
Kufuatia tukio hilo, Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu kinakemea vikali vitendo vya wananchi kujichukulia sheria mkononi na kupelekea mauaji ambayo ni kinyume na haki ya msingi ya kuishi kwa mujibu wa Ibara ya 14 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ,1977. Matukio ya wananchi kujichukulia sheria mkononi dhidi ya maafisa wa jeshi la polisi yamekuwa yakijitokeza mara kwa mara na kupelekea uvunjifu wa haki za binadamu; mnamo Oktoba 11, 2018 wanachi wa jamii ya wafugaji waliwashambulia na kuwaua askari wawili ambao walikuwa wafanyakazi wa Shirika la Hifadhi ya Taifa (TANAPA) katika hifadhi ya Ruaha iliyopo wilayani Mbarali, mkoani Mbeya.
Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu kinawakumbusha wananchi kuacha kujichukulia sheria mkononi na kufuata taratibu za kisheria katika kudai haki zao. Kwa upande mwingine LHRC inawakumbusha maafisa wa Jeshi la Polisi kuzingatia weledi katika utekelezaji wa majukumu ili kuepusha migogoro baina ya Jeshi la Polisi na wananchi. LHRC pia inaikumbusha Serikali kutengeneza mpango madhubuti wa kutatua migororo ya ardhi inayoendelea kugharimu maisha ya watanzania katika maeneo mbalimbali nchini.
Imetolewa Oktoba 23 na;
Bi. Anna Henga
Mkurugenzi Mtendaji
Unleash your inner purpose to help the helpless, marginalized and oppressed. Your contribution will help our course in provision of legal aid and promotion of human rights.
Help us curb human rights violations such as the murderous attack against people with albinism and elders.
Your donation will help us empower the general public with civic education on cross cutting issues counting gender issues and democracy to realize the changes we aspire.
Help us safeguard human rights all together.
Huenda huna muda wa kutosha wala kipato cha kutosha kulinda utu na haki za wengine, ingawa unawiwa kufanya hivyo.
Ni jukumu letu sote kujitoa kwa kidogo tulichojaaliwa ili kupaka rangi ya furaha katika nyuso za wengine, wewe, yule na sisi tukikusanya nguvu tunaweza kutetea na kulinda haki za wanaoonewa kwa kushindwa kuzifikia huduma za haki.
Jitolee sasa kidogo ulichonacho kusaidia ulinzi na utetezi wa haki na utu wa binadamu.

LEAVE A REPLY
Your email address will not be published.