Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu kimepokea taarifa za kukamatwa kwa Sheikh Ponda Issa Ponda ambaye ni Katibu Mkuu wa Shura ya Maimamu Tanzania mnamo tarehe 11 Julai, 2020.
Kwa mujibu wa taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa tarehe 14 Julai 2020 na Kaimu Katibu Mkuu Shura ya Maimamu Tanzania, Sheikh Issa Ponda alikamatwa na jeshi la polisi mnamo majira ya saa 11 jioni akiwa ofisini kwake Ilala-Dar es Salaam na kupelekwa katika Kituo cha Polisi cha Kati kwa mahojiano.
Hata hivyo, mpaka hivi sasa haijulikani Sheikh Issa Ponda anashikiliwa katika Kituo kipi cha Polisi pamoja na kuwa jeshi la polisi limekiri kumshikilia kwa mahojiano. LHRC tunasisitiza kufuatwa kwa utaratibu wa haki za mtuhumiwa kwa mujibu wa Sheria ya Mwendeno wa Makosa ya Jinai, (Sura ya 20) ya mwaka1985.
Sheria ya Mwendeno wa Makosa ya Jinai inatoa haki ya mtuhumiwa kuwasiliana na ndugu zake akiwa kizuizini, haki ya kuwasiliana na mwanasheria wake kwa wakati wote akiwa chini ya kituo cha polisi pamoja na hayo sheria hii inaweka haki ya mtuhumiwa kupata dhamana kwa kosa lolote linalodhaminika chini ya sheria hii.
Kifungu cha 30 cha Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai kinaelekeza kwamba afisa wa polisi aliemkamata mtuhumiwa wa kosa lolote anapaswa kumuachia mtuhumiwa kwa dhamana kulingana na sheria au kumfikisha mahakamani bila kuchelewa. Kifungu cha 33 cha Sheria hii kinaelekeza kuwa Mkuu wa kituo cha polisi anatakiwa kutoa taarifa mahakamani ndani masaa 24 juu ya kesi zote za watuhumiwa waliokamatwa katika mipaka ya kituo chake.
LHRC tunatoa rai kwa jeshi la polisi kuzingatia maslahi na haki za mtuhumiwa kwa mujibu wa Sheria ya Mwendeno wa Makosa ya Jinai (Sura Na. 20) ya mwaka 1985.
Imetolewa Julai 18 2020 na,
Anna Henga
Mkurugenzi Mtendaji
Unleash your inner purpose to help the helpless, marginalized and oppressed. Your contribution will help our course in provision of legal aid and promotion of human rights.
Help us curb human rights violations such as the murderous attack against people with albinism and elders.
Your donation will help us empower the general public with civic education on cross cutting issues counting gender issues and democracy to realize the changes we aspire.
Help us safeguard human rights all together.
Huenda huna muda wa kutosha wala kipato cha kutosha kulinda utu na haki za wengine, ingawa unawiwa kufanya hivyo.
Ni jukumu letu sote kujitoa kwa kidogo tulichojaaliwa ili kupaka rangi ya furaha katika nyuso za wengine, wewe, yule na sisi tukikusanya nguvu tunaweza kutetea na kulinda haki za wanaoonewa kwa kushindwa kuzifikia huduma za haki.
Jitolee sasa kidogo ulichonacho kusaidia ulinzi na utetezi wa haki na utu wa binadamu.

LEAVE A REPLY
Your email address will not be published.