Bwana Paul Revocatus Kaunda, Wakili wa Mahakama Kuu ya Tanzania amefungua kesi ya kikatiba dhidi ya Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Job Yustino Ndugai(MB), aliyekuwa Mbunge wa jimbo la Ndanda kwa tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Bwana Cecil David Mwambe pamoja na Mwanasheria Mkuu wa Serikali.
Katika kesi hiyo ya kikatiba namba 10 ya mwaka 2020; Wakili Kaunda anaiomba Mahakama Kuu kutengua amri ya Spika ya kumtambua Bwana Mwambe kama mbunge halali, ilhali Mwambe aliushautangazia umma wa watanzania ya kwamba amejivua uanachama wa chama chake cha CHADEMA na kujiunga na Chama cha Mapinduzi (CCM), kauli ambayo iliungwa mkono na katibu mkuu wa CCM, Dkt. Bashiru Ally Kakurwa aliyempokea rasmi Mwambe mbele ya hadhira kwa kumkabidhi kadi ya CCM, na Mwambe naye kumkabidhi Katibu Mkuu wake mpya kadi yake ya CHADEMA.
Wakili Kaunda amesema, kitendo cha Spika kumtambua Bwana Mwambe kama mbunge halali wakati Bwana Mwambe ameshajivua uanachama wa chama kilichomdhamini kama mbunge wa jimbo la Ndanda (2015-2020), ni ukiukwaji wa ibara ya 71(1)(f) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, 1977 na hakuna mamlaka yoyote nchini, achilia mbali Spika, yenye uwezo wa kumrudisha bungeni mbunge ambaye kwa hiari yake mwenyewe ameamua kujivua uanachama wa chama cha siasa kilichomdhamini kupata ubunge.
Kesi hiyo ya kikatiba imepangwa kusikilizwa na jopo la majaji watatu litakaloongozwa na Mheshimiwa Jaji Issa Maige. Majaji wengine ni Mheshimiwa Jaji Stephen Kirimi Magoiga na Mheshimiwa Jaji Seif Kulita.
Wakili Kaunda, katika kesi hiyo, atawakilishwa na jopo la mawakili sita litakaloongozwa na wakili mwandamizi Mpale Kaba Mpoki akisaidiwa na mawakili Daimu Halfani, Fulgence Massawe, Prisca Chogero, Stephen Msechu pamoja na Stephen Ally Mwakibolwa.
#SimamiaHaki
Kwa Jamii yenye Haki na Usawa
Unleash your inner purpose to help the helpless, marginalized and oppressed. Your contribution will help our course in provision of legal aid and promotion of human rights.
Help us curb human rights violations such as the murderous attack against people with albinism and elders.
Your donation will help us empower the general public with civic education on cross cutting issues counting gender issues and democracy to realize the changes we aspire.
Help us safeguard human rights all together.
Huenda huna muda wa kutosha wala kipato cha kutosha kulinda utu na haki za wengine, ingawa unawiwa kufanya hivyo.
Ni jukumu letu sote kujitoa kwa kidogo tulichojaaliwa ili kupaka rangi ya furaha katika nyuso za wengine, wewe, yule na sisi tukikusanya nguvu tunaweza kutetea na kulinda haki za wanaoonewa kwa kushindwa kuzifikia huduma za haki.
Jitolee sasa kidogo ulichonacho kusaidia ulinzi na utetezi wa haki na utu wa binadamu.

LEAVE A REPLY
Your email address will not be published.