Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu ni shirika binafsi, huru la hiari, lisilo la kiserikali, lisilofungamana na mrengo wowote wa kisiasa na lisiolotengeneza faida kwa ajili ya kugawana, ambalo linataamali jamii yenye haki na usawa. Kituo kina lengo la kuwawezesha watanzania ili kuendeleza, kuimarisha na kulinda haki za binadamu na utawala bora nchini.
Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu kilianzishwa mnamo Septemba 26, 1995 na wanazuoni wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, kitivo cha sheria chini ya mradi wa TANLET na baadae kusajiliwa chini ya Sheria ya Makampuni Sura na 212 ya mwaka 2002 na kufuata matakwa ya Sheria ya Asasi Zisizo za Kiserikali ya mwaka 2002.
Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu kinafuraha ya kuadhimisha miaka 23 tangu kuanzishwa kwake katika kupigania na kutetea haki za binadamu kwa lengo la kufikia jamii yenye haki na usawa. Katika miaka 23 ya utetezi wa haki za binadamu Kituo kinajivunia mafanikio kadhaa ikiwemo; kuwajengea watanzania uwezo juu ya sheria na haki za binadamu, kuwajengea uwezo wasaidizi wa kisheria zaidi ya 900 katika wilaya 30 za Tanzania bara kwa lengo la kuwezesha ufikiwaji wa huduma za haki. Pia Kituo kimeanzisha mfumo wa uangalizi wa haki za binadamu katika wilaya zote nchini ikiwa na takribani wangalizi 169 waliopo mikoa yote nchini kwa lengo la kuimarisha ulinzi wa haki za binadamu.
Katika kipindi cha miaka 23 Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu kimefanikiwa kutekeleza mambo yafuatayo;
Pamoja na mafanikio tajwa katika kipindi cha miaka 23 ya utetezi wa haki za binadamu, Kituo kimekuwa na changamoto kadhaa ikiwemo changamoto ya rasilimali watu na rasilimali fedha ili kukidhi matarajio ya wananchi. Kitendo cha Serikali kutokuelewa kazi za LHRC au kukwaza kazi za Kituo kwa makusudi ni moja ya changamoto. Katika vipindi tofauti Serikali imekuwa ikitishia na hata kuingilia moja kwa moja utendaji wa Kituo.
Tukio la Jeshi la Polisi kuvamia kituo cha uangalizi wa uchaguzi na kuwakamata maafisa wa Kituo pamoja na vifaa ikiwemo simu na kompyuta 25 zilizokuwa zikitumika kupokea taarifa za uangalizi wa uchaguzi mkuu wa mwaka 2015 bila sababu ya msingi ni mfano wa namna Serikali inavyojaribu kuzima juhudi za LHRC za kuifikia jamii yenye haki na usawa.
Changamoto nyingine ni uelewa duni wa haki za binadamu miongoni mwa wananchi ambayo hupelekea kushindwa kutofautisha kazi za Kituo na shughuli za kisiasa au vyama vya siasa. Hii hupelekea wananchi kuamini propaganda zenye lengo la kudhoofisha juhudi za Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu za kufikia Tanzania inayoheshimu misingi ya haki za binadamu na utawala wa sheria.
Kituo kinatoa wito kwa jamii, asasi za kiraia, vyombo vya ulinzi na usalama, taasisi za serikali na wadau wa haki za binadamu nchini kuendelea kukuza na kulinda haki za binadamu nchini ili kufikia jamii yenye haki na usawa.
Imetolewa Septemba 26, 2018, na;
Bi. Anna Henga (Wakili)
Mkurugenzi Mtendaji
Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu
Unleash your inner purpose to help the helpless, marginalized and oppressed. Your contribution will help our course in provision of legal aid and promotion of human rights.
Help us curb human rights violations such as the murderous attack against people with albinism and elders.
Your donation will help us empower the general public with civic education on cross cutting issues counting gender issues and democracy to realize the changes we aspire.
Help us safeguard human rights all together.
Huenda huna muda wa kutosha wala kipato cha kutosha kulinda utu na haki za wengine, ingawa unawiwa kufanya hivyo.
Ni jukumu letu sote kujitoa kwa kidogo tulichojaaliwa ili kupaka rangi ya furaha katika nyuso za wengine, wewe, yule na sisi tukikusanya nguvu tunaweza kutetea na kulinda haki za wanaoonewa kwa kushindwa kuzifikia huduma za haki.
Jitolee sasa kidogo ulichonacho kusaidia ulinzi na utetezi wa haki na utu wa binadamu.

LEAVE A REPLY
Your email address will not be published.