Katika kipindi cha wiki moja (Julai 9 -13, 2018) matukio 3 ya askari polisi kujiua yameripotiwa. Kiujumla Matukio ya watu kujiua yameendele kuwa moja ya mambo 10 yanayopelekea ukiukwaji wa Haki ya Kuishi Duniani. Sababu kuu ya askari hao kujiua inatajwa kuwa Msongo wa Mawazo (psychological stress) unaosababishwa na watu kushindwa kukabiliana na changamoto mbalimbali za kijamii kama mahusiano/ndoa, pamoja na changamoto za kiuchumi ikiwemo ugumu wa maisha. Matukio haya kwa jeshi la polisi yamekuwa ya kujirudia mara kwa mara.
Kwa mujibu wa Shirika la Afya Duniani (WHO) takribani watu laki 8 hadi milioni 1 hujiua kila mwaka kwasababu mbalimbali.
Kwa mujibu wa Sheria ya Kanuni ya Adhabu Sura ya 16, Kifungu cha 216 na 217: Kushawishi mtu Kujiua au Kujaribu Kujiua ni Kosa la Jinai. Kifungu cha 216 kinafafanua:
Mtu yeyote ambaye;
(a) anasababisha mtu mwingine ajiuwe; au (b) anamshauri mtu mwingine ajiuwe na akamshawishi kufanya hivyo; au (c) anamsaidia mtu mwingine ajiuwe, atakuwa anatenda kosa na atahukumiwa kifungo cha maisha.
Kujaribu kujiua, kifungu cha 217 kinafafanua: Mtu yeyote anayejaribu kujiua ana hatia ya kosa.
WITO KWA JESHI LA POLISI
Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu kinatoa wito kwa Jeshi la Polisi kuboresha mazingira ya kazi ya maafisa wa jeshi hilo ili kuwaepushia msongo wa mawazo unaoweza kutokana na ugumu wa maisha na mazingira ya kazi.
WITO KWA WANANCHI
Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu kinawashauri wananchi kujitahidi kuepukana na vitendo vinavyopelekea msongo wa mawazo na kuchukua hatua stahiki za utatuzi wa migogoro kijamii na kisheria.
#HakiYaKuishi ni haki ya kwanza na ya msingi zaidi kwa binadamu, tuilinde.
Unleash your inner purpose to help the helpless, marginalized and oppressed. Your contribution will help our course in provision of legal aid and promotion of human rights.
Help us curb human rights violations such as the murderous attack against people with albinism and elders.
Your donation will help us empower the general public with civic education on cross cutting issues counting gender issues and democracy to realize the changes we aspire.
Help us safeguard human rights all together.
Huenda huna muda wa kutosha wala kipato cha kutosha kulinda utu na haki za wengine, ingawa unawiwa kufanya hivyo.
Ni jukumu letu sote kujitoa kwa kidogo tulichojaaliwa ili kupaka rangi ya furaha katika nyuso za wengine, wewe, yule na sisi tukikusanya nguvu tunaweza kutetea na kulinda haki za wanaoonewa kwa kushindwa kuzifikia huduma za haki.
Jitolee sasa kidogo ulichonacho kusaidia ulinzi na utetezi wa haki na utu wa binadamu.

LEAVE A REPLY
Your email address will not be published.