Mahakama ya Afrika Mashariki kitendo cha rufaa kimepanga kusikiliza maombi ya kufuta kusudio la rufaa lililowekwa na serikali ya Tanzania katika kesi ya Sheria ya Huduma za Habari. Maombi hayo yalifunguliwa na Baraza la Habari Tanzania (MCT), Kituo cha Sheri ana Haki za Binadamu (LHRC) na Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu (THRDC). Maombi haya yatasikilizwa Mei 21, 2020 kwa njia ya mtandao (Videoconferencing) mbele ya jopo la majaji wa rufaa ya mahakama ya Afrika Mashariki ambalo litaongozwa na Raisi wa mahakama hiyo Emmanuel Ugirashebuja akisaidiana na Liboire Nkurunzinza, Aaron Ringera, Geoffrey Kiryabwire na Sauda Mjasiri.
Ikumbukwe kuwa tarehe 28 Machi 2019 Mahakama hiyo ilitoa hukumu yake na kusema baadhi ya vifungu vya Sheria ya Huduma ya Habari ya mwaka 2016 vinakiuka Mkataba unaoanzisha Jumuiya ya Afrika Mashariki na kuamuru vifutwe. Kwa kutoridhika na uamuzi wa mahakama serikali ya Tanzania ilitoa taarifa ya nia ya kukata rufaa tarehe 11 Aprili 2019 lakini mpaka leo hakuna rufaa iliyokatwa. Kwa mujibu wa kanuni za kuendesha mashauri katika mahakama hiyo serikali ilitakuwa kukata rufaa ndani ya siku 30 toka tarehe ya kuonesha kusudio la kukata rufaa.
#SimamiaHaki
Unleash your inner purpose to help the helpless, marginalized and oppressed. Your contribution will help our course in provision of legal aid and promotion of human rights.
Help us curb human rights violations such as the murderous attack against people with albinism and elders.
Your donation will help us empower the general public with civic education on cross cutting issues counting gender issues and democracy to realize the changes we aspire.
Help us safeguard human rights all together.
Huenda huna muda wa kutosha wala kipato cha kutosha kulinda utu na haki za wengine, ingawa unawiwa kufanya hivyo.
Ni jukumu letu sote kujitoa kwa kidogo tulichojaaliwa ili kupaka rangi ya furaha katika nyuso za wengine, wewe, yule na sisi tukikusanya nguvu tunaweza kutetea na kulinda haki za wanaoonewa kwa kushindwa kuzifikia huduma za haki.
Jitolee sasa kidogo ulichonacho kusaidia ulinzi na utetezi wa haki na utu wa binadamu.

LEAVE A REPLY
Your email address will not be published.