LHRC, katika kesi Miscellaneous Civil Cause No.19/2021, ilipeleka maombi Mahakama Kuu ya Tanzania, ikiomba vifungu vya Sheria ya Uchaguzi Mkuu unaohusu wabunge, madiwani na Rais, pamoja na vifungu vya Sheria ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa, vifungu ambavyo vinatoa mwanya kwa wagombea kutangazwa washindi bila kupigiwa kura na wananchi kuwa ni kinyume na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, 1977 kwakuwa inanyima haki ya wananchi kushiriki katika zoezi la uchaguzi.
Awali, kesi hiyo iliwekewa pingamizi moja na mawakili wa serikali ambapo pingamizi hilo lilikubaliwa kusikilizwa na Mahakama Kuu kwa njia ya maandishi. Baada ya pande zote kupeleka nyaraka zao mahakamani, Mheshimiwa Jaji, John Mgeta alifanya maamuzi yaliyosomwa mbele ya mawakili wa pande zote.
Jaji Mgeta amesema kwamba pingamizi hilo limekuja wakati usio wake, kwani kulifanyia kazi pingamizi hilo kutasababisha kwenda kwenye kiini cha kesi ya msingi, kinyume na utaratibu wa mapingamizi ya awali unavyotaka. Pingamizi hilo la serikali limetupiliwa mbali na kesi ya msingi itaendelea kuskilizwa.
Imetolewa na;
Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu
Unleash your inner purpose to help the helpless, marginalized and oppressed. Your contribution will help our course in provision of legal aid and promotion of human rights.
Help us curb human rights violations such as the murderous attack against people with albinism and elders.
Your donation will help us empower the general public with civic education on cross cutting issues counting gender issues and democracy to realize the changes we aspire.
Help us safeguard human rights all together.
Huenda huna muda wa kutosha wala kipato cha kutosha kulinda utu na haki za wengine, ingawa unawiwa kufanya hivyo.
Ni jukumu letu sote kujitoa kwa kidogo tulichojaaliwa ili kupaka rangi ya furaha katika nyuso za wengine, wewe, yule na sisi tukikusanya nguvu tunaweza kutetea na kulinda haki za wanaoonewa kwa kushindwa kuzifikia huduma za haki.
Jitolee sasa kidogo ulichonacho kusaidia ulinzi na utetezi wa haki na utu wa binadamu.

LEAVE A REPLY
Your email address will not be published.