Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) kimefuatilia kwa ukaribu changamoto zinazoendelea nchini kwa ukosefu wa maji. LHRC inatoa rai kwa serikali kufanya jitihada za haraka kutatua shida ya maji iliyopo sasa. Ibara ya 14 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, 1977 inaweka haki ya uhai ambapo, bila maji safi na salama haki hii haitoweza kufikiwa. Hivyo, serikali inawajibu wa kuhakikisha wananchi wake wanapata maji safi na salama.
Mgao wa maji umeendelea kuleta athari za kiuchumi kwa wafanyabiashara, kijamii kwa wananchi kwa ujumla, kiusalama na kiafya hasa kuchochea visababishi vya magonjwa ya mlipuko katika jamii hasa kwa kundi la watoto na wanawake.
Ni ukweli kwamba, ukosefu wa maji unaendelea kutesa watoto na wanawake kwa kutembea umbali mrefu kutafuta maji hata kipindi cha usiku. Hali hii inachochea vitendo ukatili dhidi ya wanawake na watoto kwa kuongeza migogoro ya kifamilia.
LHRC inatoa wito kwa Serikali kuchukua mikakati ifuatayo;
Mikakati ya muda mfupi
Mikakati ya muda mrefu
Imetolewa leo tarehe 18 Novemba 2021 na;
Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC)
Anna Henga (Wakili)
Mkurugenzi Mtendaji
Unleash your inner purpose to help the helpless, marginalized and oppressed. Your contribution will help our course in provision of legal aid and promotion of human rights.
Help us curb human rights violations such as the murderous attack against people with albinism and elders.
Your donation will help us empower the general public with civic education on cross cutting issues counting gender issues and democracy to realize the changes we aspire.
Help us safeguard human rights all together.
Huenda huna muda wa kutosha wala kipato cha kutosha kulinda utu na haki za wengine, ingawa unawiwa kufanya hivyo.
Ni jukumu letu sote kujitoa kwa kidogo tulichojaaliwa ili kupaka rangi ya furaha katika nyuso za wengine, wewe, yule na sisi tukikusanya nguvu tunaweza kutetea na kulinda haki za wanaoonewa kwa kushindwa kuzifikia huduma za haki.
Jitolee sasa kidogo ulichonacho kusaidia ulinzi na utetezi wa haki na utu wa binadamu.

LEAVE A REPLY
Your email address will not be published.