TAMKO LA KULAANI MAUAJI YA YA ASKARI POLISI MKOANI ARUSHA YALIYOFANYWA NA RAIA
Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu kimepokea kwa masikitiko makubwa taarifa za mauaji ya kikatili yaliyofanywa kwa Askari Polisi wa Kituo kidogo cha Polisi Mbughuni ajulikanae kama PC Damas siku ya tarehe 23/7/2021 wakati akitekeleza majukumu yake. Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu kinalaani kitendo hiki ambacho kimekiuka haki ya kuishi ya PC Damas.
Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu kinatoa rai kwa wananchi kuwa ni vyema wananchi wote wafahamu kwamba Askari Polisi wapo kwa mujibu wa sheria na kazi yao kubwa ni kulinda usalama wa raia na mali zao. Siyo jambo la busara kwa wananchi kuwashambulia maaskari wanapokuwa wanatekeleza majukumu yao kwani kwa kufanya hivyo ni kujaribu kuwaficha wahalifu na hivyo kuchochea ongezeko la vitendo vya uhalifu katika jamii zetu.
Ni matumaini ya Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu kwamba Serikali itachukua hatua za makusudi kuhakikisha kwamba aliyefanya tukio ya mauaji ya PC Damas anatafutwa na kuchukuliwa hatua za kisheria.
Imetolewa leo Julai 26, 2021
Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu
Anna Henga (Wakili)
Mkurugenzi Mtendaji
Unleash your inner purpose to help the helpless, marginalized and oppressed. Your contribution will help our course in provision of legal aid and promotion of human rights.
Help us curb human rights violations such as the murderous attack against people with albinism and elders.
Your donation will help us empower the general public with civic education on cross cutting issues counting gender issues and democracy to realize the changes we aspire.
Help us safeguard human rights all together.
Huenda huna muda wa kutosha wala kipato cha kutosha kulinda utu na haki za wengine, ingawa unawiwa kufanya hivyo.
Ni jukumu letu sote kujitoa kwa kidogo tulichojaaliwa ili kupaka rangi ya furaha katika nyuso za wengine, wewe, yule na sisi tukikusanya nguvu tunaweza kutetea na kulinda haki za wanaoonewa kwa kushindwa kuzifikia huduma za haki.
Jitolee sasa kidogo ulichonacho kusaidia ulinzi na utetezi wa haki na utu wa binadamu.

LEAVE A REPLY
Your email address will not be published.