TAARIFA KWA UMMA
Kesi ya kupinga tozo ya miamala ya simu iliyofunguliwa na Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) shauri la namba 11 la mwaka 2021 imesikilizwa leo kwa mara ya pili saa nne (4) asubuhi mbele ya Mheshimiwa Jaji John Mgeta katika Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Dar es Salaam.
Kesi hiyo imesikilizwa ambapo mawakili wa upande wa serikali wameweka mapingamizi yakiomba kuifuta kesi hiyo kwa madai ya kwamba kesi hiyo haina mashiko. Mapingamizi hayo matatu yaliyoletwa na upande wa serikali unadai:
(iii) Madai hayo yamekosa ruhusa ya bodi ya mdai (Board Resolution).
Mahakama imesikiliza mapingamizi hayo ambapo upande wa serikali uliwakilishwa na Wakili Mkuu wa Serikali Wakili Gabriel Malata na upande wa mlalamikaji uliwakilishwa na Wakili Mpale Mpoki.
Kesi hiyo imepangwa tena tarehe 08/09/2021 ambapo mahakama itatoa uamuzi kuhusu mapingamizi hayo.
Imetolewa leo Agosti 18, 2021 na;
Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC)
Bi. Anna Henga (Wakili)
Mkurugenzi Mtendaji
Unleash your inner purpose to help the helpless, marginalized and oppressed. Your contribution will help our course in provision of legal aid and promotion of human rights.
Help us curb human rights violations such as the murderous attack against people with albinism and elders.
Your donation will help us empower the general public with civic education on cross cutting issues counting gender issues and democracy to realize the changes we aspire.
Help us safeguard human rights all together.
Huenda huna muda wa kutosha wala kipato cha kutosha kulinda utu na haki za wengine, ingawa unawiwa kufanya hivyo.
Ni jukumu letu sote kujitoa kwa kidogo tulichojaaliwa ili kupaka rangi ya furaha katika nyuso za wengine, wewe, yule na sisi tukikusanya nguvu tunaweza kutetea na kulinda haki za wanaoonewa kwa kushindwa kuzifikia huduma za haki.
Jitolee sasa kidogo ulichonacho kusaidia ulinzi na utetezi wa haki na utu wa binadamu.

LEAVE A REPLY
Your email address will not be published.