Ni takribani miaka 23 tangu kuanzishwa kwa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu. Katika kipindi hicho chote Kituo kimekua kikiendesha programu mbalimbali za elimu ya Haki za Binadamu ikiwemo kupigania kuwepo kwa Katiba Mpya ya nchi inayoakisi maoni ya wananchi. Tanzania iliamua kuanza uandishi wa katiba mpya kutokana na kua katiba zote tano zilizopita tangu katiba ya uhuru ya mwaka 1961 mpaka katiba ya kudumu ya mwaka 1977 pamoja na marekebisho yake yote 14 vimekuwa vikilalamikiwa kwa kutoshirikisha wananchi kikamilifu. Hivyo ukaundwa mfumo ambao ungeruhusu ushiriki wa wananchi katika kupata katiba bora.
Pamoja na kukwama kwa kwa mchakato wa mabadiliko ya katiba mnamo mwezi Aprili 2015 ambao ulianzishwa mnamo mwaka 2011, bado Kituo kinaamini kuwa kuna umuhimu mkubwa na wa haraka wa kuendeleza mchakato huo kutokana na sababu mbalimbali.Kwa kutambua umuhimu huo, Kituo kimeona umuhimu wa kuandaa kitabu hiki kidogo ambacho ni zao la ripoti ya uchambuzi mkubwa wa kina uliofanywa na wataalam wa masuala ya Katiba na Sheria kutoka chuo kikuu cha Dar es Salaam. Kitabu hiki kinaweka bayana mambo makuu mawili ambayo ni sababu kuu za kukwama kwa mchakato wa katiba; na mapendekezo ya njia nzuri za kuufufua na kuendeleza mchakato wa Katiba ambao unabeba maoni ya wananchi.
Ni matumaini yangu kwamba kitabu hiki kitachangia kukuza uelewa wa wananchi juu ya sababu za mkwamo wa mchakato wa Katiba na njia ambazo zinapendekezwa kuchukuliwa katika kuendeleza mchakato wa Mabadiliko ya Katiba kwa kuzingatia maoni ya wananchi. Soma hapa RIPOTI MAALUM JUU YA MKWAMO WA MCHAKATO WA KATIBA MPYA
Dkt. Helen Kijo - Bisimba
Mkurugenzi Mtendaji
Unleash your inner purpose to help the helpless, marginalized and oppressed. Your contribution will help our course in provision of legal aid and promotion of human rights.
Help us curb human rights violations such as the murderous attack against people with albinism and elders.
Your donation will help us empower the general public with civic education on cross cutting issues counting gender issues and democracy to realize the changes we aspire.
Help us safeguard human rights all together.
Huenda huna muda wa kutosha wala kipato cha kutosha kulinda utu na haki za wengine, ingawa unawiwa kufanya hivyo.
Ni jukumu letu sote kujitoa kwa kidogo tulichojaaliwa ili kupaka rangi ya furaha katika nyuso za wengine, wewe, yule na sisi tukikusanya nguvu tunaweza kutetea na kulinda haki za wanaoonewa kwa kushindwa kuzifikia huduma za haki.
Jitolee sasa kidogo ulichonacho kusaidia ulinzi na utetezi wa haki na utu wa binadamu.
